Kiswahili hivi sasa ni lugha inayotumiwa na watu wapatao milioni 300 katika Afrika Mashariki na Kati kama nyenzo ya mawasiliano ya siku kwa siku. Wengi wa watumiaji hawa hutumia lugha nyengine pia zenye asili ya ndani ya Afrika au hata zile zilizo na asili ya Bara hilo kama vile Kiingereza na Kifaransa. Kwa wengi pia, Kiswahili si lugha yao ya kwanza na kwa baadhi hata ya pili siyo.
Ajabu lakini ni pale wote hao wanapojipa haki ya kuwa, kujitambua na kukidai Kiswahili kuwa ni chao. Ndipo wengine hujiuliza, hivi kwani hiki Kiswahili hakina mwenyewe?
Na jibu ni kuwa kinao. Si kila mtumiaji wa Kiswahili anazungumza Kiswahili, na hata anapotokea kukizungumza, bado si kila azungumzaye Kiswahili ni Mswahili. Kiswahili kinao wenyewe na wenyewe ni Waswahili.