Our writings do not only define what we are and how we perceive the world around us but they also are an image of ourselves that will remain many years after we have departed this world.

Mohammed Ghassani

“Tangu hapo nikagundua kuwa nimekutana na mshairi chipukizi gwiji, mwenye kipawa kikubwa chenye mwangwi wa kazi za washairi maarufu wa Kiswahili. Kazi za akina Muyaka bin Haji Al-Ghassany, Abdilatif Abdalla,  Ahmad Nassir wa Mvita, na akina Kamange na Sarahani wa Pemba.” – Kwenye Machozi Yamenishiya: Diwani ya Mohammed Ghassani

Profesa Said A. M. Khamis

Tukiviacha vitambulisho vya isimu zake, Mohammed Ghassani ana vipaji vinavyomfanya awe na vitambulisho vingine tafauti: mshairi, mtangazaji wa redio ya kimataifa, mwanahabari, mwandishi, mpiga picha, mchapishaji vitabu na gwiji wa mitandao ya kijamii. Kwa ufupi, na kwa hakika, yeye ni taasisi kamili. Ni taasisi ya mtu mmoja yenye kukhusika na tasnia ya mawasiliano, kwa upana wake wote.

Ahmed Rajab