
Tuacheni utashi wa maslahi binafsi na tuwekeni mbele utashi wa maslahi ya umma zaidi. Dk. Shein na Maalim Seif, wawili nyinyi ndio tuliowachagua kushika dola mwaka 2010 ili mtuongoze kwa amani na tuende kwa amani katika kila hatua tunayopita. Kaeni kwa pamoja kama wewe Maalim Seif na Rais Karume mulivyokaa awali, na kwa msaada wa Kamati ya Maridhiano, hadi mkafanikiwa kufanya uchaguzi wa aina yake kwa Zanzibar. Ni uchaguzi wa 2010 tu ndio uliokosa kumwaga damu hata tone moja.
Continue reading “Wanaoapa kutotoa nchi kwa ‘vikaratasi’ wapime kasi ya wimbi”