Sir James Mancham alikuwa rais wa kwanza wakati Seychelles inapata uhuru wake mwaka 1976, lakini akapinduliwa mwaka mmoja tu baada ya kuingia madarakani katika mapinduzi ambayo mwenyewe anaituhumu Tanzania kuhusika. Ismail Jussa anatupitisha kwenye kurasa za kitabu alichokiandika mwanadiplomasia huyo wa kimataifa kuelezea maisha yake: Seychelles Global Citizen.
Continue reading “TUFUNUWE KITABU: Seychelles Global Citizen cha Sir James Mancham”Tag: Tanzania
LULU ZA ZANZIBAR: Kanali Ali Mahfoudh, kamanda wa ukombozi mashariki na kusini ya Afrika
Bi Naila Majid Jidawi mwenye umri wa miaka 77, anasimulia kuhusu mumewe, Marehemu Kanali Ali Mahfoudh, aliyezaliwa na kukulia Zanzibar, akapata mafunzo ya kijeshi Cuba na akawa miongoni mwa walioshiriki kuipindua serikali ya uhuru ya Zanzibar mwaka 1964, lakini akafungwa miaka kumi jela kwa tuhuma za mauaji ya Mzee Abeid Karume na akachukuliwa na Rais Samora Machel wa Msumbiji akiwa mshauri mkuu wa masuala ya ulinzi na vita vya ukombozi mashariki na kusini mwa Afrika.
TUFUNUWE KITABU: Abeid Karume (1905-1972)
Leo, Ismail Jussa anatuchambulia kitabu cha wasifu wa Rais wa Kwanza wa Zanzibar, Sheikh Abeid Karume, kupitia kitabu cha Ali Shaaban Juma.
TUFUNUWE KITABU: Mafunzo kutoka “Pan-Africanism or Pragmatism?” cha Prof. Issa Shivji
Wiki iliypota, Ismail Jussa alichambua kitabu cha “The Partner-ship: Miaka 30 ya Dhoruba” kilichoandikwa na Marehemu Aboud Jumbe Mwinyi, na leo anachambua cha Profesa Issa Shivji, Pan-Africanism or Pragmatism?”, ambacho ni muakisiko wa kile cha Marehemu Jumbe.