KISWAHILI KINA WENYEWE

Ni “tanzia” au “taazia”?

_dsc1163Chembelecho (au chambilecho, au chambacho) msemo wa Kiswahili, “Kipya kinyemi, kingawa kidonda.” Ni dasturi ya baadhi ya watu kuvutiwa na kipya kitokacho kwengine, hata kama tangu hapo wanacho chao wenyewe kifananacho na hicho cha kigeni. Hili swala la maneno kama “mubashara” lina tanzu mbili. Utanzu wa kwanza ni huo wa kupenda kukimbilia maneno  ya kigeni, hata kama tunayo yetu wenyewe yenye maana hiyo hiyo. Kama ilivyokwisha elezwa, kabla ya habari “mubashara” tumekuwa tukisema habari/ ripoti za moja kwa moja, au za papo kwa papo (wala si “papo” pekee).

 

Continue reading “Ni “tanzia” au “taazia”?”

KISWAHILI KINA WENYEWE

Ni “kiasi cha…” sio “kiasi ya…”

AbdilatifKwa uchache wa nifahamuvyo, lugha fasaha ni kusema “kiasi cha…”, basi haidhuru iwe ni kwa watu au kwa vitu. Yaani, kiasi cha watu kumi, au kiasi cha miti kumi. Kama  ambavyo twasema, kitabu cha…, kisa cha…, kiatu cha…, kitambo cha…, na kadhalika, wala hatusemi kitabu ya…, kisa ya…, kiatu ya…, wala kitambo ya… Na ni hivyo kwa sababu maneno yote hayo yamo katika ngeli ya KI/VI. Basi ikiwa kwa maneno hayo niliyoyatolea mfano hatuyatumilii “ya”, kwa nini iwe kwa neno “kiasi”?

Continue reading “Ni “kiasi cha…” sio “kiasi ya…””

KISWAHILI KINA WENYEWE

Kitenzi ‘piga’ na ladha yake

Kiswahili kina ladha yake. Hapana shaka ni lugha zote, ingawa kwetu hili ndilo titi la mama, halishi hamu. Kitenzi ‘piga’ kinaweza kuonekana kuwa na maana mbaya katika hali yake ya awali, maana humaanisha ‘shambulia’, ‘dhuru’, ‘umiza’ na mengine yenye mshindo kama huo. Continue reading “Kitenzi ‘piga’ na ladha yake”