Bi Naila Majid Jidawi mwenye umri wa miaka 77, anasimulia kuhusu mumewe, Marehemu Kanali Ali Mahfoudh, aliyezaliwa na kukulia Zanzibar, akapata mafunzo ya kijeshi Cuba na akawa miongoni mwa walioshiriki kuipindua serikali ya uhuru ya Zanzibar mwaka 1964, lakini akafungwa miaka kumi jela kwa tuhuma za mauaji ya Mzee Abeid Karume na akachukuliwa na Rais Samora Machel wa Msumbiji akiwa mshauri mkuu wa masuala ya ulinzi na vita vya ukombozi mashariki na kusini mwa Afrika.
Tag: Karume
CCM Z’bar haina uhalali kujinasibisha na Mapinduzi
Ukizingatia hotuba za Marehemu Mzee Abeid Karume na matendo yake wakati wa uhai wake, ukazingatia marudio ya kauli za Marehemu Karume kupitia kwa mjane wake, Mama Fatma Karume, ukasikiliza hotuba moja tu ya Mheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha aliyoitoa katika moja ya mikutano yake na wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), moja kwa moja unapata maana na malengo halisi ya Mapinduzi ya Zanzibar ya tarehe 12 Januari 1964 na kisha unahitimisha kuwa mshirika mkuu kwenye Serikali ya Umoja wa Kitaifa Zanzibar, yaani CCM, yuko mbali kabisa na malengo ya Mapinduzi hayo na, hivyo, amepoteza kabisa uhalali wa kujinasibisha nayo.
Continue reading “CCM Z’bar haina uhalali kujinasibisha na Mapinduzi”