BLOG POSTS, ZANZIBAR DAIMA PUBLISHING

Dhuluma Iliyodumu na Kudamirisha

Mwaka wa nane sasa huu, Wazanzibari walio wengi wamekataa kushawishika kuwa viongozi wa Uamsho wanaoshikiliwa na dola walitenda kosa lolote linalotajwa na dola hiyo. Kwa miaka yote hii minane, msimamo wao umesalia kuwa ule ule mmoja: kwamba hii ni dhuluma ya kisiasa iliyotendwa kwao na adhabu waliyobebeshwa kwa niaba ya Wazanzibari wenzao. Walipelekwa “wakanyelee ndooni” (kwa maneno ya Balozi Seif Ali Iddi) ili liwe funzo kwa wengine wenye mtazamo wa kisiasa waliokuwa wakiuhubiri viongozi hawa hadharani – msimamo wa ZANZIBAR HURU.

Continue reading “Dhuluma Iliyodumu na Kudamirisha”
UCHAMBUZI

Lissu wa dhahabu

Mkononi mwangu nina kitabu kiitwacho ‘A Golden Opportunity? Justice & Respect in Mining’ (Fursa ya Dhahabu? Haki na Heshima kwenye Madini) cha mwaka 2008. Waandishi wake ni wawili – Mark Curtis na Tundu Lissu. Ni matokeo ya utafiti uliofanywa na wawili hao wakiwa chini ya Baraza la Wakristo Tanzania (CCT) na Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) na uchapishaji wake kufadhiliwa na Shirika la Misaada la Kikristo la Norway. Continue reading “Lissu wa dhahabu”