BLOG POSTS

Zanzibar Reconciliation (Episode 1): A Chat with Lawyer Awadh on the Controversy

The decision by ACT Wazalendo to join the Government of National Unity in Zanzibar after the October 2020 fraud elections has caused fierce discussions between supporters and opponents, both within and outside the party. In particular, this chat is about the debate between supporters of the decision in Zanzibar and the opponents from the main opposition party in Tanzania Mainland, CHADEMA. The former president of Zanzibar Law Society, Awadh Ali Said, joins me in the chat.

UCHAMBUZI

Lissu wa dhahabu

Mkononi mwangu nina kitabu kiitwacho ‘A Golden Opportunity? Justice & Respect in Mining’ (Fursa ya Dhahabu? Haki na Heshima kwenye Madini) cha mwaka 2008. Waandishi wake ni wawili – Mark Curtis na Tundu Lissu. Ni matokeo ya utafiti uliofanywa na wawili hao wakiwa chini ya Baraza la Wakristo Tanzania (CCT) na Baraza la Waislamu Tanzania (BAKWATA) na uchapishaji wake kufadhiliwa na Shirika la Misaada la Kikristo la Norway. Continue reading “Lissu wa dhahabu”

UCHAMBUZI

Bila ya nguvu za dola na vurugu, CCM wepesi

Naandika makala hii refu baada ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Robert Manumba, kujitokeza wiki mbii zilizopita kuwaasa viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), hasa wenyekiti Freeman Mbowe na Kaimu Naibu Katibu Mkuu Zitto Kabwe, kwamba wachunge kauli zao maana zinaweza kuwaweka pabaya kwa vile zina muelekeo wa kuvunja amani. Amani na utulivu ni misamiati ya kijanja inayotumika na Chama cha Mapinduzi (CCM) na mawakala wake kujijengea taswira kwamba wao ni watu wastaarabu, ilhali ni kinyume chake. Naamini naye DCI Manumba amezungumza zaidi kisiasa kuliko ‘kiulinzi’. Continue reading “Bila ya nguvu za dola na vurugu, CCM wepesi”