Kwa uchache wa nifahamuvyo, lugha fasaha ni kusema “kiasi cha…”, basi haidhuru iwe ni kwa watu au kwa vitu. Yaani, kiasi cha watu kumi, au kiasi cha miti kumi. Kama ambavyo twasema, kitabu cha…, kisa cha…, kiatu cha…, kitambo cha…, na kadhalika, wala hatusemi kitabu ya…, kisa ya…, kiatu ya…, wala kitambo ya… Na ni hivyo kwa sababu maneno yote hayo yamo katika ngeli ya KI/VI. Basi ikiwa kwa maneno hayo niliyoyatolea mfano hatuyatumilii “ya”, kwa nini iwe kwa neno “kiasi”?
Tag: afrika mashariki
Nimtoweje zizini?
Ni mkubwa mtihani, alouzusha nguruwe
Aliye asi zizini, yeye na maswahibuwe
Kuingiza ufitini, watakalo lao liwe
Nimtoweje zizini, nguruwe aliyeasi? Continue reading “Nimtoweje zizini?”