BLOG POSTS, BOOKS, eBOOKS, KISWAHILI KINA WENYEWE, PAPERBACK, ZANZIBAR DAIMA PUBLISHING

Mfalme Yuko Uchi: Diwani Mpya ya Mohammed Ghassani

NJOO uniulize Mohammed Khelef Ghassani ni nani na nitakupa vitambulisho vyake kadhaa. Kila kimoja kati yavyo kitamsibu.  Kitajaa kama pishi. Continue reading “Mfalme Yuko Uchi: Diwani Mpya ya Mohammed Ghassani”

KISWAHILI KINA WENYEWE

Wapi neno mwanana hutumika?

abdilatif_abdalla_2Mtu mwanana, mti mwanana, upepo mwanana, LAKINI Kiswahili chanana, nyumba nyanana. Mzizi wa sifa hii ni -anana. Kwa hivyo, inahitaji kiambishi awali cha jina la kitu kinachopawa sifa. Najua kwamba kuna wengi watumiao “mwanana” kwa kila ngeli. Kwa maoni yangu, hicho si Kiswahili fasaha.

Continue reading “Wapi neno mwanana hutumika?”

KISWAHILI KINA WENYEWE

Ni “tanzia” au “taazia”?

_dsc1163Chembelecho (au chambilecho, au chambacho) msemo wa Kiswahili, “Kipya kinyemi, kingawa kidonda.” Ni dasturi ya baadhi ya watu kuvutiwa na kipya kitokacho kwengine, hata kama tangu hapo wanacho chao wenyewe kifananacho na hicho cha kigeni. Hili swala la maneno kama “mubashara” lina tanzu mbili. Utanzu wa kwanza ni huo wa kupenda kukimbilia maneno  ya kigeni, hata kama tunayo yetu wenyewe yenye maana hiyo hiyo. Kama ilivyokwisha elezwa, kabla ya habari “mubashara” tumekuwa tukisema habari/ ripoti za moja kwa moja, au za papo kwa papo (wala si “papo” pekee).

 

Continue reading “Ni “tanzia” au “taazia”?”