Kabla ya kuelezaa maana ya neno “mwanamajumui”, kuna mambo mawili ambayo ni muhimu kuyaeleza. La kwanza, ni kwamba kuna wasemao “mwanaumajumui”; na baadhi ya watu huidondosha hiyo u walitumiapo neno hilo. Continue reading “Kuhusu Mwanamajumui”
Tag: abdilatif abdalla
Kibaruwa
Kwenye shamba hilo kubwa asilani hakunyi mvuwa
Ni kwa mitilizi ya jasho langu ndiyo hunweshezewa
Kwenye shamba hilo kubwa sasa imeshaiva kahawa
Na bunize ni matone ya damu yangu niliyotowa
Ndipo mte ukatipuza Continue reading “Kibaruwa”
Baina ya mkandarasi na kandarasi – 2
Nimetangulia kusema kwamba hayo niliyoyaeleza kabla hayakuwa yamenishughulisha sana kwa sababu, mtu aweza kuwa na hiari ya kutumia maneno kandarasi/makandarasi au mkandarasi/wakandarasi, akusudiapo kuwa ni mtu. (Mimi nitaendelea kutumia kandarasi/makandarasi – tena bila ya wasiwasi wowote!) Continue reading “Baina ya mkandarasi na kandarasi – 2”
Baina ya mkandarasi na kandarasi – 1
Mmojawapo miongoni mwa washairi maarufu wa Tanzania, Khamis Amani Nyamaume (1926-1971), katika shairi lake labeti nne, liitwalo ‘Saa’, alitunga akasema:
Saa za huku na huko, zimekosana majira
Sababu ni mzunguko, haufuati duara
Sasa rai iliyoko, ni kubadilisha dira
Saa zatupa majira, mafundi zitengezeni… Continue reading “Baina ya mkandarasi na kandarasi – 1”