Marehemu Aboud Jumbe Mwinyi ndiye aliyekuwa rais wa pili wa Zanzibar baada ya Mapinduzi ya 1964 na akaja kuondolewa na Mwalimu Julius Nyerere mwaka 1984 katika kile kinachoitwa “Kuchafuka Hali ya Hewa ya Kisiasa Zanzibar”. Miaka 10 baadaye alichapisha kitabu chake kinachozungumzia sakata zima la yeye kuondolewa madarakani na kuelezea msimamo wake juu ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Ismail Jussa anatupitisha kwenye kurasa zake kuchota mafunzo yaliyomo.
Category: UCHAMBUZI
Makala na uchambuzi wa Mohammed Ghassani
TUFUNUWE KITABU: Mafunzo kutoka The Asian Aspiration
Kitabu cha The Asian Aspiration kilizinduliwa mwishoni mwa mwezi Julai 2021 visiwani Zanzibar, na miongoni mwa wageni 50 waliohudhuria kwenye uzinduzi huo ni Ismail Jussa, ambaye kwenye Silsila hii ya kwanza anatudondolea baadhi ya mafunzo ambayo Zanzibar inaweza kujifunza kutoka mataifa ya Asia kuelekea maendeleo na ustawi wa watu wake.
Ninaishi Magharibi
Continue reading “Ninaishi Magharibi”Kwa lugha na utamaduni wangu, magharibi ina maana nyingi: ndiko jua linakotulia likaibadilisha leo kuwa jana na kuitayarisha kesho kuwa leo. Ndicho kielelezo pia cha kumalizika kwa maisha ya mwanaadamu ya hapa duniani, maana magharibi kawaida huja na giza, na giza ni alama ya mauti. Magharibi pia ni nadharia ya kisiasa kwenye medani za kilimwengu na lugha yangu imeipokea hivyo hivyo – kuwa ni mataifa ya Ulaya na Marekani yanayoambiwa yameendelea kiuchumi, kisiasa na kijamii.
Uhusiano baina ya ukosefu wa demokrasia na kushamiri kwa ufisadi
Uchambuzi huu unakusudia kuonesha – kwa nadharia – uhusiano mkubwa uliopo baina ya ukosefu wa demokrasia na kushamiri kwa ufisadi. Hoja ni kwamba kadiri demokrasia inavyokosekana ndivyo ufisadi unavyojiimarisha na kisha nao ufisadi ukazuwia demokrasia kufanya kazi yake.
Continue reading “Uhusiano baina ya ukosefu wa demokrasia na kushamiri kwa ufisadi”