NJOO uniulize Mohammed Khelef Ghassani ni nani na nitakupa vitambulisho vyake kadhaa. Kila kimoja kati yavyo kitamsibu. Kitajaa kama pishi. Continue reading “Mfalme Yuko Uchi: Diwani Mpya ya Mohammed Ghassani”
Category: KISWAHILI KINA WENYEWE
Sarufi, Fasihi, Ushairi, Uchambuzi wa Lugha ya Kiswahili
Kuhusu Mwanamajumui
Kabla ya kuelezaa maana ya neno “mwanamajumui”, kuna mambo mawili ambayo ni muhimu kuyaeleza. La kwanza, ni kwamba kuna wasemao “mwanaumajumui”; na baadhi ya watu huidondosha hiyo u walitumiapo neno hilo. Continue reading “Kuhusu Mwanamajumui”
Kiswahili kina wenyewe, kienee lakini kisitokomee
Utangulizi
Kama zilivyo lugha nyingi zilizopata bahati ya kuwa kiunganisho baina ya wazungumzaji kutoka makabila na mataifa mengine, Kiswahili nacho kina wenyewe wenye asili nacho na kina watumiaji wa kawaida. Continue reading “Kiswahili kina wenyewe, kienee lakini kisitokomee”
Kibaruwa
Kwenye shamba hilo kubwa asilani hakunyi mvuwa
Ni kwa mitilizi ya jasho langu ndiyo hunweshezewa
Kwenye shamba hilo kubwa sasa imeshaiva kahawa
Na bunize ni matone ya damu yangu niliyotowa
Ndipo mte ukatipuza Continue reading “Kibaruwa”
Sahihi ni Ipi: Sala au Swala?
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
رَبِّ اشْرَحْ لِي صَدْرِي ﴿٢٥﴾ وَيَسِّرْ لِي أَمْرِي ﴿٢٦﴾ وَاحْلُلْ عُقْدَةً مِّن لِّسَانِي ﴿٢٧﴾ يَفْقَهُوا قَوْلِي
Ewe Mola wangu Mlezi! Nikunjulie kifua changu, Na unifanyie nyepesi kazi yangu, Na ulifungue fundo lililo katika ulimi wangu, Wapate kufahamu maneno yangu. (Suratu Maryam Aya ya 25-28)
UTANGULIZI
Mimi si mtaalamu wa lugha, wala si mweledi katika uandishi. Sikuondokea kujishughulisha na kazi ya uandishi, na bahati mbaya mpaka sasa nimebaki vivyo hivyo. Japokuwa sina ufasaha pia katika uzungumzaji, lakini huwa ninafadhilisha kufikisha makusudio yangu kwa njia ya uzungumzaji kuliko uandishi. Kwa sababu hiyo, nimekuwa nikitembea nalo kichwani mwangu kwa muda mrefu, dukuduku langu la haya nitakayoyaeleza katika andiko hili, mpaka hivi karibuni ilipotokea sababu ya heri iliyonipa msukumo wa kukaa kitako na kuchapa maneno haya. Continue reading “Sahihi ni Ipi: Sala au Swala?”
TUPO: Diwani ya Tungo Twiti
Naamini kuwa hii ni kazi ya kwanza ya tungo ya mashairi ya Kiswahili kuandikwa katika ukamilifu wa kitabu kupitia mkusanyiko uliotokana na kuandikwa katika mtandao wa kijamii wa Twitter. Na kama ndivyo basi roho na moyo wangu ni burdan kwa kuwa mtangulizi katika hili. Continue reading “TUPO: Diwani ya Tungo Twiti”
Kilio cha Usumbufu: Diwani mpya ya Kiswahili inayoangazia majanga ya kijamii
Ikiwa ni vigumu kusema kwa kinywa kipana ushairi ni nini, si vigumu kamwe kulitambua shairi zuri ni lipi. Mara unapolikabli (au tuseme linapokukabili), hukuvaa kwa nguvu za ajabu na kukupenya kwa hisia ya raha isiyoweza kuelezeka. Continue reading “Kilio cha Usumbufu: Diwani mpya ya Kiswahili inayoangazia majanga ya kijamii”