KISWAHILI KINA WENYEWE

Wapi neno mwanana hutumika?

abdilatif_abdalla_2Mtu mwanana, mti mwanana, upepo mwanana, LAKINI Kiswahili chanana, nyumba nyanana. Mzizi wa sifa hii ni -anana. Kwa hivyo, inahitaji kiambishi awali cha jina la kitu kinachopawa sifa. Najua kwamba kuna wengi watumiao “mwanana” kwa kila ngeli. Kwa maoni yangu, hicho si Kiswahili fasaha.

Nilipokuwa mdogo, nilikuwa nikiwasikia wazee wakiitumia sifa hiyo, -anana, kwa vitu vinavyohisika, vinavyodirikika, au vinavyoonekana kwa akili au kwa hisia. Kwa mfano, upepo mwanana (upepo unaopuliza  kwa upole na utulivu); sauti nyanana (sauti nzuri inayopendeza masikioni na kuburudisha); ngozi nyanana (ngozi nyororo); maji manana (maji yaliyotuwama au kutiririka kwa upole); mtu mwanana (mtu mpole, mwenye tabia nzuri na maingiliano mazuri na wenziwe).
Ni katika utuuzimani mwangu ndipo nilipoisikia sifa hiyo ikitumiliwa karibu kila kitu. Ndipo tukawa twasikia, au kusoma, nyumba nyanana, gari lanana, na kadhalika.
Hayo ndiyo niwezayo kuyaeleza kwa ufupi.

3 thoughts on “Wapi neno mwanana hutumika?”

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.