KISWAHILI KINA WENYEWE

Kibibi

Pafukapo moshi, moto wakaribia
Kipwagacho jikoni,mezani chasubiriwa
Kieleacho baharini, pwani kitawadia
Hakuna liso mwisho, toka zama daharia

Chema kisitrini, tuhali kuharibia
Mwendo kama tausi, shwari yake tabia
Sie hasa afiriti, vya watu kuvidowea
Hakuna liso mwisho, toka zama daharia

Kibibi wetu mzuri, kwa sifa katimilia
Mwendo wake na sauti, katimia malkia
Rangi yake zifuri, mwendo wake wa ngamia
Hakuna liso mwisho, toka zama daharia

Wamsemao kwa chuki, kwa kweli wamkosea
Kweli kasoro hakosi, aloumbwa na jalia
Ila mwamtia nyingi dhiki, mabaya kumzulia
Hakuna liso mwisho, toka zama daharia

Mulosema si kweli, afiriti mumezua
Ati kakwapua mali, sio yake ilokuwa
Kwa ushahidi lukuki, muloleta kupalilia
Hakuna liso mwisho, toka zama daharia

Mlosema yamejiri, asilani  kumtokea
Kwa viapo na takbiri, mupate kuaminiwa
Awe kiumbe dhalili, kwa watu  jumuiya
Hakuna liso mwisho, toka zama  daharia

Amedhirisha Jalali, ya uongo mlozua
Haikumfika idhilali, mulopanga kumtia
Imewafika simanzi, aibu kubwa ya dunia
Hakuna liso mwisho, toka zama daharia

Azuliwaye maiti, hawezi kujitetea
Hukumu yake siratwi, kwa Mola wetu Jalia
Huko ‘tapewa haki, kila alodhulumiwa
Hakuna liso mwisho , toka zama daharia

Suleiman Shaaban Suleiman 
23 Agosti 2016

1 thought on “Kibibi”

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.