Wataalamu na wachambuzi wa fasihi wanakipa umuhimu mkubwa kipengele cha sitiari (uhamishaji wa sifa kutoka kitu kimoja kwenda chengine) miongoni mwa tamathali za semi katika fasihi. Kuna ambao wanafikia umbali wa kuhoji kuwa ni kipengele hiki pekee ambacho kinaweza kuipa uhai kazi ya fasihi na kuifanya isimame kwenye maana halisi. Sikiliza hapa mhadhara wa Profesa Kulikoyela Kahigi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mbele ya Kongamano la 29 la Kiswahili la Bayreuth, kusini mwa Ujerumani.
https://soundcloud.com/mohammed-k-ghassani/matumizi-ya-sitiari-katika-ushairi-prof-kahigi