‘Mengia Lata na N’guza, wakidai wao Mungu
Nasi bila kuchunguza, tukavaa zao pingu
Sasa wanatutatiza, kwa idhara na virungu
-
Miujiza walisema, tutaiona harakaWagonjwa wangesimama, na wafu wangefufuka
Nyati angekuwa kima, na simba akawa paka
Edai neema Lata, majumbani zitajaaShida tutaitafuta, na raha zitatuvaaYote hatukuyapata, labda nyingi balaa
Simba amekuwa paka, na paka hajulikaniNyati kageuka nyoka, atambaa majaniniKima juu anashuka, ataka kazi za ndani
Bata amekuwa chui, na ng’ombe kawa peleleKuku hawafi kwa ndui, wamalizwa na uzileNa mdudu buibui, ala shina na viale
N’guza ataka tutii, kwa kadiri apendavyoLakini hayajutii, mambo yetu Kenda ovyoWanyonge hasaidii, wanabaki hivyo hivyo
Kwa nguvu Lata adai, tumpe sijida zetuAnasema hawajui, Mola na Mtume wetuLakini hayaondoi, mabaya yalofurutu
N’guza yeye atunyima, tusile ashibe yeyeAtesa hata wanyama, hajali hata nduguye‘Kimhoji utamkoma, kusema ukujutiye
Lata adai na nguvu, ahuuwisha akifisha‘Kisema ana ubavu, makubwa kuyadogoshaAtia watu makovu, wanyonge aadabisha
N’guza atwaa ya kwake, na yaliyomzungukaVyote wiwe chini yake, tumuombe tukitakaNi bahari tumbo lake, lazibeba hata taka
Jichole lina mtoto, Lata haoni vizuriJapo mwembamba kya fito, vazi lake ni kiburiKwa maneno ya mkato, Lata yeye ni tajiri
N’guza japo anaona, rangi zote hazijuiKwake zote za fanana, nyeupe na baibuiKazi yake kutubana, vyetu vimo havikui -
-
-
Ng’uza atisha wavyele, kwa visu na hiziraniAtaka wote walale, ahodhi vlivyo ndani
Wabakie vile vile, na kazi yao ya mwani
Wadai tuwahamidi, hata kama zumbukukuKubwa wafanya juhudi, tutii zao shaukuKuwakana sina budi, si Mungu ni makhuluku
Wote hawana amana; wakisema hawatendiYa ukweli wayakana, uungwana hawapendiWabaya wao ni wana, wakusanya kwa makundi
Wao si wakamilifu, ndio mana nawabezaNa wala singii hofu, wito wao kupuuzaKatwaani siwasifu, japo kwenu ‘tachukiza
Kasoro zao zi wazi, kila mtu azijuaNi viumbe wa Azizi; na hili walitambuaMungu hawi na kizazi, na sifa ya kupunguaMaalim Mussa
23 Februari 2016
Zanzibar
-