KISWAHILI KINA WENYEWE

Lata na Ng’uza

‘Mengia Lata na N’guza, wakidai wao Mungu
Nasi bila kuchunguza, tukavaa zao pingu
Sasa wanatutatiza, kwa idhara na virungu

  • Miujiza walisema, tutaiona haraka
    Wagonjwa wangesimama, na wafu wangefufuka

    Nyati angekuwa kima, na simba akawa paka

     

    Edai neema Lata, majumbani zitajaa
    Shida tutaitafuta, na raha zitatuvaa

    Yote hatukuyapata, labda nyingi balaa

     

    Simba amekuwa paka, na paka hajulikani
    Nyati kageuka nyoka, atambaa majanini

    Kima juu anashuka, ataka kazi za ndani

     

    Bata amekuwa chui, na ng’ombe kawa pelele
    Kuku hawafi kwa ndui, wamalizwa na uzile

    Na mdudu buibui, ala shina na viale

     

    N’guza ataka tutii, kwa kadiri apendavyo
    Lakini hayajutii, mambo yetu Kenda ovyo

    Wanyonge hasaidii, wanabaki hivyo hivyo

     

    Kwa nguvu Lata adai, tumpe sijida zetu
    Anasema hawajui, Mola na Mtume wetu

    Lakini hayaondoi, mabaya yalofurutu

     

    N’guza yeye atunyima, tusile ashibe yeye
    Atesa hata wanyama, hajali hata nduguye

    ‘Kimhoji utamkoma, kusema ukujutiye

     

    Lata adai na nguvu, ahuuwisha akifisha
    ‘Kisema ana ubavu, makubwa kuyadogosha

    Atia watu makovu, wanyonge aadabisha

     

    N’guza atwaa ya kwake, na yaliyomzunguka
    Vyote wiwe chini yake, tumuombe tukitaka

    Ni bahari tumbo lake, lazibeba hata taka

     

    Jichole lina mtoto, Lata haoni vizuri
    Japo mwembamba kya fito, vazi lake ni kiburi

    Kwa maneno ya mkato, Lata yeye ni tajiri

     

    N’guza japo anaona, rangi zote hazijui
    Kwake zote za fanana, nyeupe na baibui
    Kazi yake kutubana, vyetu vimo havikui
  •  

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.