KISWAHILI KINA WENYEWE

Ni Mpwa Wetu Huyu!

Mie kwanza kwa isimu
Kumzukuru karimu
Alie iumba damu
Mwilini katembea

Ni yeye mwenye uweza
Alo ipanua chaza
Kwenye mkondo wa kiza
Lulu kaibarikia

Nimshukuru rabana
Hazawa nami nmwana
Kwenye visiwa mwanana
Jinale zinjibaria

Huwaingia majonzi
Wapitao na jahazi
Hawana hata ushanzi
Katika vyetu visiwa

Nafsi zawatamani
Ijapo iwe zamani
Mababu arubaini
Apate pakuungia

Kwa kua nsifa nno
Sie kuzaliwa huno
Inakua ni nfano
Duniani watolewa

Azuke karibu nasi
Ajitie ukakasi
Atupake makamasi
Huku akiturandia

Ajioneshe nfano
Eti kan’zongwa nno
Apenda nshikamano
Mahaba yakumuua

Aupenda aung’ariza
Akilala auwaza
Asubuhi ang’aruza
Ungalipo au laa.

Aje atushupalie
Kwasifa atusifie
Kwa ghera asimamie
Tusiseme lilo sawa

Yumkini ntu huyu
Yumo akaanga mbuyu
Nwawapi bwana huyu
Mbona kutubururia?

Ikanishia tamaa
Haiwi awe jamaa
Akatuletea haaa
Huyu wakutumiliwa

Hikaa mepumbuwaa
Fikira zimenijaa
Nikashituli haaaaa!
Huyu si wakudandia

N’wetu wa mwilini
Kapotelea porini
Karudi kuja tukhini
Damuye ilomzaa

Huyu si wa kule nno
Mbali vidole vitano
Huhitaji  malumbano
Atojapo wapajua

Nikajirudisha nyuma
Kupekura nlosoma
Nazinga ile heshima
Mbona inanipotea?

Nikaunga unga doti
Sikupata tofauti
Mwenye kuku kwenye koti
Kashaaza kumyea

Eeeeh mola mtenze nguvu
Usimpe ushupavu
Akatupaka utonvu
Urimboni kututia

Ishamwishia tamaa
Karudi kujikalia
Wale walomtumia
mbwembwe wanamtilia

Yarabi usimkhini
Na kuchi wake kotini
Ende nae kaburini
Siku atayo jifia.

Atoya
2015

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.