KISWAHILI KINA WENYEWE

Mungu Atabaki Mungu

Viko vya kufananisha, angani na nchi kavu, lakini si Mungu
Mbona wajiaibisha, mchana jua angavu, kiumbe kumwita Mungu
Dunia imeshakwisha, hali sasa si tulivu, nawambia walimwengu

Uongozi ni wadhifa, anayetoa ni Mungu, hakuna asiyejua
Sio kuleta maafa, kumpa sifa ya Mungu, huku ni kujiumbua
Kukufuru sio sifa, ni madhambi kwa mafungu, dhoruba iso mvua

Polisi si malaika, kamwe yeye hafanani, ni kiumbe mpungufu
Hufanya analotaka, hata kama la dhambini, cheo kipate turufu
Malaika kasifika, hata kwenye Qur-ani, ametajwa na Raufu

Msahafu haufanani, na katiba ya kiumbe, kkitabu kitakatifu
Wala injili yashani, havina kasoro chembe, ni vitabu vya Raufu
Taurati ya zamani, vitabu vyenye ujumbe, mwongozo mbainifu

Na Zaburi ya Daudi, dahari ilidhihiri, ikiwa imetimia
Wapate kuyafaidi, kuyatambua ya kheri, maasi kuyabagua
Vipi unajifisidi, wabadili tafsiri, uzushi watuletea

Mitume si mawaziri, usijitie pumbao, kwa mifano iso macho
Unaona ni fakhari, kuwasifu wenye vyeo, watengeza chakulacho
Jua tu kwenye safari, kaburini ni kituo, utavuna upandacho

Kila ashangiriaye, alichosema mwenzetu, ajuwe hasalimiki
Sote pamoja na yeye, ‘tarudi kwa Mola wetu, kwa shime tujishitaki
Maneno tuyafukie, toba iwe nguzo yetu, Mola atatuafiki
Ally Hilal
Wete – Pemba

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.