KISWAHILI KINA WENYEWE

Mbazi Chakula Gani Mgeni Kukirimiwa?

Mbazi chakula gani, mgeni kukirimiwa?
Nazitoke ugenini, nchini zikaingia
Zikainjikwa jikoni, kachanua kama ua
Zikaweka mezani, zikafunikwa na kawa
Ukaalikwa mgeni, sahani ukajaziwa
Hunabudi mgeni, kula moja kama dawa
Mbaazi chakula gani, mgeni kukirimiwa?

Wanaopenda mbaazi, hii ni hasara yao
Japo ni kitu azizi, kwa sifa na mila zao
Sitajitia ajizi, hashiriki mwendo wao
Kwangu kuzila mbaazi, sawa kuwa na wao
Mungu sinipe mapenzi yakufata mwendo wao
Siwezi katu siwezi, naogopa watu hao
Mbaazi chakula gani mgeni kukirimiwa?

Chakula hiki jamani, hadi uchotee upawa
Kinanipa kisirani, wakila bila kunawa
Walaji wake jamani, ukiwaona ‘tajuwa
Akizaliwa kwetu ndani, au mgeni ikawa
Kingine hawakioni, chakula wakavutiwa
Mbaazi kwao mbaazi, ndicho wanachojuwa
Mbaazi chakula gani, mgeni kukirimiwa?

Said Miraaj Abdulla
Dar es Salaam

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.