KISWAHILI KINA WENYEWE

Wana waniwana

Najisikia furaha, kuwa nawanwa ni wana
Nyumbani ninapongia, kelele ‘kapigishana
Wakaanza salimia, kwa salam ziso jina
Ila huwa naridhia, kuona miye nawanwa

Wana waniwaniapo, wakaanza pakatana
Wakakaa nikaapo, nyajihi kutazamana
Tukafanya vichekesho, vya baba na wake wana
Hapo ndipo nipendapo, kuwa nawanwa ni wana

Waniwania kwa hamu, kwa pamoja himahima
Hawataki panga zamu, wakawa wapokezana
Kwa misingi ya nidhamu, wawana tukawanana
Na mapenzi yakadumu, baba kuwanwa ni wana

Hamad Hamad
5 Septemba 2013
Zanzibar

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.