KISWAHILI KINA WENYEWE

Siamini Niotayo

Zenji yetu yatoweka, yatoweka naiona
Ndio ndoto nnoota, usiku hata mchana
Ndoto hii yanifata, nendako yaniandama
Siamini nnoota, sitamani kuyaona

Naota kila kukicha, habari huwa nasoma
Mitandaoni napita, yalojiri kuyaona
Zenji nyumbani kwapwita, shuari haiko tena
Kuchafu kumechafuka, si shuari si salama

Bahari inachafuka, naota meli zazama
Roho zinapukutika, mikondoni zinkwama
Walio juu wacheka, hiyo kwao ni neema
Na waliosababisha, habari hata hawana

Makasri ya shubaka, yalojengwa kwa gharama
Yaloipatia sifa, Zenji dunia nzima
Naota yaporomoka, mengine ngoda yanama
Taratibu yanyofoka, naota Zenji si njema

Naota mwitu wawaka, joto hilo laririma
Jozani yayayatika, joshi juu laparama
Faya zipo zishafika, moto haziwezi zima
Mbuga, wanyama na nyika, ma’lesh havipo tena

Naota watu wabweka, wabwekea wao wana
Wana wanapoinuka, kutoa chao kyalima
Kupinga wasichotaka, kwa chema wanachoona
Wana kiapo ‘meapa, n’go hawarudi nyuma

Nayaota makanisa, yanajaa isilama
Misikiti yafurika, kiristu mejazana
Kila mtu kajiweka, pasipo pake kwa jina
Mambo yamechanganyika, naona vyangu nakama

Mnadani yanadishwa, nchi hivi naiona
Madalali wana hisa, bei wapunguziana
Naona mwisho shafika, Zenji hiyo yayoyoma
Sekunde zahisabika, Zenji haiyetu tena

Nakataa kuamka, bora nilale daima
Niendelee kuota, yasijiri niloyona
Kwa maana hiamka, tashindwa kulala tena
Nalala sebu amka, ukweli sebu uona

Hamad Hamad
12 Februari 2013
Copenhagen

4 thoughts on “Siamini Niotayo”

  1. Mimi nafikir jibu tunalo.ila naamin Mungu yupo.na hakubali waja wake wadhulumiwe hasa waco na hatia.shair zuri lina maana.

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.