KISWAHILI KINA WENYEWE

Chawa Sasa Uondoke!

Chawa sasa huna budi , uniondoke kichwani
Uwe na mimi baidi, japo kuwa umachoni
Nafanya hivi kusudi, kunusuru langu ini
Chawa uuke kichwani ijapo umeshitadi

Kweli wenitia hamu, wakati nilikinywani
Nekuwa mwendawazimu, hijiona namba wani,
Kumbe waninyonya damu, sasa nimeshabaini
Chawa uuke kichwani, wakati usalazimu

Niiona fahari, chawa kweli siutani,
Ela nazidi kariri, niache nitaabani
Tena ‘sifanye kiburi, kwamba wekubaliani.
Nataka utamakani, jambo hili le hiari
Wakati siwako tena, nakuonea imani
Huna tena la kunena, likangia sikioni
Uka dunia ni pana, kwengine ukazaini
Chawa uuke kicheani, sikuyo imewadia

Said O.  Shoka
Zanzibar

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.