KISWAHILI KINA WENYEWE

Nikuwinde Hadi Lini?

Nikuwinde hadi lini, niipate salamuyo
Wanikimbiya kwa nini, kunifanyia uchoyo
Wajua nimapenzini, utosi hadi unyayo
Ndio ukatenda hayo

Ningojee hadi lini, kuuona wajihiwo
Wajikimbiza gizani, waruka huna kituo
Hikuuliza kwa nini, wanamba nitabiayo
Wanijua taumiya

Wataka nifanye nini, niipate kauliyo
Unambiye ukenami, nami nipate pumuo
Nga’ hiuzwa n’waani, n’jidai mmaliyo
Sininyime nitakayo

Hamad Hamad
21 Disemba 2012
Copenhagen

3 thoughts on “Nikuwinde Hadi Lini?”

  1. Ndugu yangu si pekeyo, mfano wako ni wengi.
    Yashanikuta mwenzio, hetaka kuvuta bangi.
    Nilianzaia Bweleo, nikafika hadi Nungwi.
    Sababu mtoto huyo, nampenda hanipendi.
    Kwanini?

    Kwanini najiuliza, sababu yake sioni.
    Azidi kunitatiza, hanitoki mawazoni.
    Kila nikimuuliza, anikataa kwa nini?
    Ashindwa kujieleza, ni kama hana ulimi.
    Nashangaa..!

    Nashangaa akipita, namuuliza hasemi.
    Chochote anachotaka, akitaje kwangu mimi.
    Penzi lake kulikosa, kwangu ni umasikini.
    Kwangu hataki kuckeka, tabasamu silioni.
    Nisaidieni…..

    Nisaidieni nyote, kwa rai na kwa hekima.
    Huyu binti nimpate, niwe Baba awe Mama.
    Mawazo nipumzike, mwenzenu mechoka sana.
    Niliseme jina lake? mupate kumuandama?
    Naumia..

    Naumia si utani, homa gonjwa la kitoto.
    Mapenzi yapo moyoni, anijia kwenye ndoto.
    Natamani afueni, nipoe na hili joto.
    Kwa vilivyo duniani, huyu kwangu ndio pepo.

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.