KISWAHILI KINA WENYEWE

Kwa Jinalo Zanzibari

Kwa jina la Zanzibari, uhuru tuliupata
Uhuru ulobashiri, Zanzibar kuneemeka
Mwezi wa kumi na mbili, sitini na tatu mwaka
Na UN tukafika

Kwa jina la Zanzibari, uhuru tukaja pokwa
Mapinduzi Januari, ndicho kilichofanyika
Tukanza upya safari, kwenda tusikokutaka
Tukaanza taabika

Kwa jina la Zanzibari, mapinduzi yakatekwa
Kwa mungano uso kheri, Unguja na Tanganyika
Tukawa kama sifuri, nchi iso mamlaka
Ndipo hapa tupo sasa

Kwa jina la Zanzibari, uhuru mpya twataka
Mpya wa kujiamuri, tufanye tunavyotaka
Tusivutwe kwa shemeri, tuwe baidi na nyika
Twataraji tutafika

Kwa jina la Zanzibari
Uhuru tuliupata
Uhuru tukaja pokwa
Mapinduzi yakatekwa
Uhuru mpya twataka
Inshaallah tutaupata

Hamad Hamad
15 Disemba 2012
Copenhagen

1 thought on “Kwa Jinalo Zanzibari”

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.