KISWAHILI KINA WENYEWE

Uraisi si Rahisi

Ndoto yangu ya awali, ya kutaka uraisi
Sasa n’shaibadili, siuwezi najihisi
Uraisi si akili, si elimu si ukwasi
Siwezi kuwa Raisi

Uraisi ni kiburi, kwa maana yetu sisi
Kufanya watu dhalili, kuwageuza vinyesi
Kuwadhoofisha hali, bila ya hata kisisi
Sitaki kuwa Raisi

Dhuluma huwa sukani, ya kuiendesha nchi
Kuwanyonya masikini, kuwapora zao haki
Kuwatia hatiani, na kuwabambika kesi
Nachelea Uraisi

Uraisi ni khiyana, miadi kuikhalifu
Mwanzoni unoyasema, kwa ulimi mnadhifu
Mwishoni waja yakana, kwa matendoyo machafu
Uraisi si rahisi

Jisahau nachelea, nikija kuwa Raisi
Kutuma watu kuuwa, kupiga na kunajisi
Sababu kubwa kwa kuwa, hawetaka nifuasi
Siutaki uraisi

Kuwa Raisi mwongozwa, sitaki sitadiriki
Sitaki kutumilizwa, ni wasiositahiki
Hawa mbwa hasumizwa, nitende kile na hiki
Siuwebu Uraisi

Nakichelea kiapo, cha kugwia msahafu
Cha kukazanisha macho, hajifanya sina khofu
Nacha pazwa hagwa papo, haja habopwa n’tutu
Kuwani nyie raisi

Hamad Hamad
4 Novemba 2012

Copenhagen

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.