KISWAHILI KINA WENYEWE

Kikombe

Mfanowe sijaona, kikombecho duniani
Chenye heba ya maana, na shepu ya wastani
Katu hakijafanana, na chochote kwa uzani

Kina marembo ya shani, na umbo lilotonona
Mitumko ya pembeni, tumtum imetuna
Na makiye ukingoni, burda metulizana

Kikishikwa chashikana, chatulia mkononi
Hakipwayi chajibana, kikajaa kiganjani
Sitaki kisifu sana, haja kitoa thamani

Kidole kimebaini, raha inopatikana
Kingiapo mkononi, mwa kikombe kikazama
Kikenda juu na chini, mdomoni kwa kupima

Kikombe nnokisema, si cha kahawa jamani
Sicho mnachokiona, kwa macho yenu ‘tamani
Ni kikombe nnochona, kwa jicho la hisiani

Hamad Hamad
Copenhagen
06-09-2012

1 thought on “Kikombe”

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.