KISWAHILI KINA WENYEWE

Kutafsiri neno na sio maana

Mtihani mmoja ninaokabiliana nao katika kufanya kazi ya uandishi wa habari kwenye chombo cha kimataifa, ni kutafsiri taarifa kutoka lugha za kigeni, kama Kiingereza na Kijerumani, kuja lugha ya Kiswahili. Na ni mtihani si kwa sababu ya uwezo mdogo kwa lugha hizo, bali kutokana na ukweli kuwa lugha ni kielelezo cha tamaduni na maana ambayo watu wa utamaduni fulani huyapa mambo na dhana katika maisha yao.

Matokeo yake ni kwamba ni.nadra sana kukuta pana tafsiri ya neno kwa neno kutoka lugha moja kwenda nyengine, hasa inapotokea kuwa lugha hizo zinawakilisha tamaduni zinazopishana sana kijiografia, kiimani na kiteknolojia. Mtu asipozingatia ukweli huu, ndipo anapoishia kulazimisha matumizi ya misamiati kuwasilisha dhana ambazo hazieleweki kwa walengwa. Kwa mfano, utasikia mtangazaji anasema: Rais wa Guinea alikufa pale ‘akipokea’ matibabu Ufaransa.

Hiyo ni tafsiri ya neno kwa neno
ya “the Guinean president died while receiving medical treatment in France.” Lakini mantiki ya lugha ya Kiswahili haikubali tafsiri hii. Kwa mfano inataka patumike tafsida ya ‘kufariki au kuaga dunia’ badala ya neno kavu ‘kufa’ na sio ‘pale akipokea’ bali wakati akipatiwa matibabu, maana kwa utamaduni wa Kiswahili matibabu hayapokewi ila hupatikana.

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.