KISWAHILI KINA WENYEWE

Kisima cha Peke Yangu

Nipokee mshairi, kwa moyo wa maridhia
Niji na langu shauri, moyoni nimelitoa
Mungu ’takulipa kheri, na ubora wa afia
Nimekiweka cha kwangu, nipate kukata kiu

Ninatokea safari, kusaka mafanikio
Sijatembea kwa gari, silo langu kusudio
’Taonekana jeuri, kukosa matarajio
Nimekiweka cha kwangu, nipate kukata kiu

Lengo langu ni kisima, kilicho cha peke yangu
Hata kama nusu pima, lakini kiwe cha kwangu
Sitaki jirani mwema, nikiteke peke yangu
Nimekiweka cha ndani, nipate kukata kiu

Tele huko majiani, visima na sivitaki
Hata kwa wangu jirani, na maji hayakauki
Kiu yangu kisirani, kamwe hainiondoki
Nimekiweka cha ndani, nipate kukata kiu

Hivyo vina kamba nyingi, kila mtu mchotaji
Huchotwa bila msingi, na wenye kiu ya maji
Hata akiwa kidingi, mradi awe mywaji
Nimekiweka cha ndani, nipate kukata kiu

Wataniita mchoyo, ila silo lengo langu
Kuchanganya na mwenzio, sitokyeta tena changu
Na kiu niliyonayo, haitotoka wenzangu
Nimekiweka cha ndani, nipate kukata kiu

Nisameheni wenzangu, chimbeni vil’o vya kwenu
Kisima cha peke yangu, sitochota vilo vyenu
Niikate kiu yangu, za kwenu shauri zenu
Nimekiweka cha ndani, nipate kukata kiu

Suleiman Mkubwa (Tajiri wa Ushauri)
27 Disemba 2011
Zanzibar

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.