KISWAHILI KINA WENYEWE

Kama Nini Maanaye

Mtu ameulizia, maana ya KAMA NINI
Mimi kwanza namwambia, lugha sio yake fani
Mana angelitambua, maana ya kama nini
Kama nini maanaye mithiliye huioni

Ukisema yu aavyaa, yu avyaa kama nini
Maana anavyovaa, mfanowe huuoni
Toto anazitotoa, nyingi zisizo kifani
Kama nini maanaye, mithiliye huioni

Mfano watu wa Kae, kanikaza kama nini
Maana ampendae, mithiliye huioni
Anampenda tujuwe, mwenginewe hatamani
Kama nini maanaye, mithiliye huioni

Hapo mtaposikia, kuna kura ya maoni
Basi msijekosea, muwe wengi kama nini
Muwe wengi kama nini, yetu yaende usoni
Kama nini maanye, mithiliye huioni

Nadhani atatambua, maana ya kama nini
Tamati ninafikia, naondoka darasani
Somo nimempatia, mifano imesheheni
Kama nini maanaye, mithilite huioni

Hapa tena sitaraji, mbele mimi kusogea
Naondoka Sir Haji, kwengine naelekea
Kitu ninachotaraji, jawabu imetulia
Kama nini maanaye, mithiliye huioni

Mzee Haji (Sir Haji)
24 Novemba 2011

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.