KISWAHILI KINA WENYEWE

Hatupati kwa Utashi

Wengi tunavitamani, vile vilo kiririni
Tuvitie mkononi, tuseme sasa shuwari
Lakini ni hamkani, tena kikiri kikiri
Hatupati kwa utashi

Kweli tunavyotamani, vingi tunastahiki
Lakini vimikononi, mwa wenye kutudhihaki
Wao huwa farahani, kihisi twapata dhiki
Hatupati kwa utashi

Mija na moja ni tatu, babu alituambia
Sijui hesabu zetu, wapi tunaelekea
Kama ni za babu zetu, au twageuza njia
Hatupati kwa utashi

Mjini na vijijini, mimi ninawashtua
Kwa haraka amkeni, tuanze kujitetea
Tusiwe vibarazani, uwanjani twakimbia
Hatupati kwa utashi

Bila matendo aushi, haja zetu hazijiri
Hatupati kwa utashi, hata vitu vya hiari
Hupata kwa ushawishi, bidii pia dhamiri
Hatupati kwa utashi

Sir Haji nishasema nadhani mumesikia
Kama ndio himahima, mbele tungesogelea
Waume na kinamama, hakuna wakubakia
Hatupati kwa utashi

Mzee Haji

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.