KISWAHILI KINA WENYEWE

Mauti Yanifikapo

Zama Mauti nifika, nikaitwa na Rabbuka, papo hajifia,
Zamu yangu imefika, Kaburini nikizikwa, nanyi mkinifukia,
Mkimaliza mwauka, mwaniacha weweseka, kwa upweke lonachia,
Habakia milenia, Dua njema kwimbiwa!

Zeraili kinijia, roho yangu jitwalia, namimi papo heliya,
Nakumbuka swahibia, dunia lowaachia, na wao wefurahiya,
Najua nenda mkiwa, sena wa kunifatia, nikawa nae pamoya,
Kwavyo newa Masikini!

Siku watu wanizika, kesha wenda pumzika, keniacha mpwekeya,
Kiifikiri nayuta, matendo ovu futika, na dhuluma itendeya,
“Ngeweza ngeimarika, akhera nikiishika, kiighiriki duniya”
Mayuto kila hayuta, Hakuna nosaidia!

Siku hiyo ni nzito, wafungwa kama kipeto, watupwa kijachiliya,
Wageuka ni mtoto, waliya bila kipato, hakuna we kuombeya,
Msaada ulonacho, saidizi wa mkato, matendo mema tendeya,
Naiogopa Milele, siku hiyo ifikapo!

Kwangu mwana Ali Haji, kujinusuru khitaji, mema nikijitendeya,
Dhuluma nisikhitaji, maovu siwe mtaji, kwayo nikajilemaya,
Nirejele kwa Mumbaji, msamaha nitaraji, huenda tasameheya,
Nijiandalie sasa, maisha ya Milenia!!!!!

By,
Othman Ali Haji,
20/11/2011,
Zanzibar.

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Twitter picture

You are commenting using your Twitter account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.