KISWAHILI KINA WENYEWE

Enenda!

‘Lidhani ‘tajikalia, kisubiri yako huba, kwayo uliyonitenda!
‘Takaa nikinyamaa, ‘kingoja yako suhuba, na mwili wangu ‘kikonda!
Chakula ‘tajimia, mai katu setashiba, kikufikiri kipendwa!
Kamwe siwi hayawani, enenda sirudi tena!!!

Enenda huko ‘tomea, kamwe kwangu nakwambia, “enenda katu serudi”!
Enenda nakuapia, sitawa mwana mkiwa, kwamba sina mburudi,
Tena nakuhakishia, nafasiyo ijaziwa, neshalipata waridi,
Enenda sejirudishe, sina haja nawe kamwe!

Enenda sijerudia, sifikiri tajiua, kukosa wako usudi,
Kama ulifikiria, kienda wewe tajuya, na kujiua tasudi,
Ukidhani haramia, takiteka kwa ubuya, na sasa tajihusudi,
Ulijidanganya sana!

Nakwamba nekuhakiya, fahamu sijeumiya, kwangu tena ‘serudi,
Sina pa kukuekeya, na moyo wangu hemiya, tena nazidi shadidi,
Ubakile hedithiya, athari kwangu sekoya, na kamwe haitarudi,
Enenda sirudi tena!

Othman Ali Haji,
20/11/2011,
Zanzibar.

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.