KISWAHILI KINA WENYEWE

Nataka Nende Nyumbani

Nataka nende nyumbani, haone wangu wavyele
Haanze walo Ziwani, Shengejuu hadi Ole
Hashibishe zao mboni, nami moyo utulile
Mola wangu niauni, lengo langu nifikile

Nataka nende nyumbani, hajikumbushe ya kale
Hakae msikitini, niwepo safu ya mbele
Hitakiwa niadhini, haraka bila sumile
Nende na maulidini, hale haluwa mabale

Nataka nende nyumbani, niliyako hasikizwa
Ngolengole midomoni, hichagiza hachombezwa
Hakorogewa ngaani, hap’wa sheli lya kupwazwa
Habwagwa vyangu chagoni, taratibu kwa kulazwa

Nataka nende nyumbani, hagowezane na watu
Gowe si la miilini, kuwana gowe papatu
Shitizai na matani, ndio silika ya kwetu
Hisha nirudi nyumbani, halumbe na wanakwetu

Nataka nende nyumbani, haonane na’lo wangu
Wangu kwa nje na ndani, wangu wa tangu na tangu
Wangu wa usingizini, wangu wa tamu na chungu
Lini tafika nyumbani, hatimize ndoto yangu?

Hamad Hamad
15 Juni 2011
Copenhagen

2 thoughts on “Nataka Nende Nyumbani”

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.