KISWAHILI KINA WENYEWE

Hamkani

Dhoruba hii hakika, huchukua na kuzoa
Kwa wenye kubahatika, na kwa kipaji Jalia
Seuze wa tikatika, na wale mazoa zoa
Nani atabakia?

Imekuwa patashika, angani na bara pia
Watu wanahangaika, wapi watakimbilia
Kila mtu anataka, njia kujisafishia
Nani atabakia?

Usiku wahangaika, mchana wauchelea
Mbu huwa kwao shaka, hawajali malaria
Kusudi kunusurika, na janga la zahania
Nani atabakia?

Wapo wanomithilika, majabari wa dunia
Walizani wamefika, safari waloanzia
Hafla inatikisika, gari walioingia
Nani atabakia?

Tarehe ikitajika, huzunini huingia
Wanazidi taabika, shuwari inapotea
Kwa kweli wamahanika, na janga la zahania
Nani atabakia?

Najua mwapapatika, jawabu kunipatia
Katu si yangu dhihaka, kuona nasimbulia
Kwani ninachokitaka, najua mushatambua
Nani atabakia?

Amaan, Masoud Bakar
17 Mei 2011
Zanzibar

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.