KISWAHILI KINA WENYEWE

Salata

Uliniahidi, kwamba wenipenda ‘tanitumikia
Ukaitakidi, kuwa ‘tanilinda na kunitetea
Iwapi ahadi, mbona kushapinda wanigeukia?

Uliniapia, kwa Muumba wako hakuaminia
Nkasherekea, mikononi mwako mie kunitia
Sikufikiria, kwa tamko lako haya ‘ngenambia

Wejikubalisha, kwa khiyari yako ukanichukua
Sekukalifisha, ni utashi wako us’o na kinaa
Leo wanirusha, si changu ni chako kila ulotwaa?

Uliniambia, kila nitakacho utanipatia
Nkakutajia, ni hichi na hicho nakihitajia
Kumbe hwesikia, kunkuwa kocho wanimon’gonyoa?

Nekukaribisha, himayani mwangu mie hajiviza
Hakutawalisha, kila kilo changu uweze kitunza
Kushakinadisha, na kibanda changu wataka kiuza?

Sistahamili, kwa salata yako macho hafumbia
Napanga kitali, nikufate kuko nije kudungua
’Choka ufidhuli, na kiburi chako unonifanyia

Hamad Hamad
15 Mei 2011
Copenhagen

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.