Siku ikifika, tajifunga lemba
Nipite hicheka, kina hijigamba
Furaha hakika, itavunja myamba
Siku ya furaha
Siku hiyo hasa, ndio siku yangu
Ya kusema sasa, nami mlimwengu
Zama zimekwsiha, kumeza machungu
Siku ya furaha
Tapiga miluzi, nyote musikiye
Mupate maizi, furaha siriye
Munipe pongezi, munikumbatiye
Siku ya furaha
Siku naingoja, na yakaribiya
Siku ya faraja, ya kusherekeya
Sitaki itaja, ‘taniharibiya
Siku ya furaha
Hamad Hamad
7 Mei 2011
Copenhagen
Naijile naijile, hima isijechelewa
‘Sichelewe ifikile, sikuyo akhi ikawa
Ikawa yangu ja vile, lyako n’ lyangu kwa kuwa
Kwa kuwa tushaamuwa, hili nalo tuchangile
siku hiyo ikifika, kake siache nambia
siku hiyo ya baraka, kweli inakaribia
jitayarishe kudaka, la kwangu takupatia
sote tutafurahika, ewe mola jaalia
siku hiyo babake, nami tafurahia
tatamba kwa makeke, wote tajionea
tamrushi mateke, yule ataejinamia
nami tafurahia, ewe mola jaalia