KISWAHILI KINA WENYEWE

Fakhari ya Uswahili

Si wa hili u wa lipi, uso tambua utuo
Wajitambulisha vipi, kuilinda heshimayo
Moyo wangu haunipi, kuvaa si yangu nguo
Huu ndio uswahili, kwawo najifakharisha

Najifakharisha kwayo, fakhari ya Uswahili
Tatanga kila kituo, hapa ndipo manzili
Na mwisho wa zangu mbio, ‘tanikuta Zanzibari
Huu ndio uswahili, kwawo najifakharisha

Naona fakhari sana, kula kwa mkono wangu
Si kwa vijiko na nyuma, nikajifanya mzungu
Maamkizi ya heshima, nawapa wakubwa wangu
Huu ndio uswahili, kwawo najifakharisha

Lugha ni kubwa bahati, Mola aliyotupayo
Siwezi kuisaliti, haipenda nyingineyo
Yanibeba kitikiti, naipigia chapuo
Huu ndio uswahili, kwawo najifakharisha

Na mswahili ni yupi, kama si wa Zanzibari
Kwengine ni kapikapi, hapa ‘sa ndio asili
Sikusudii dhihaki, nachonga watu ukali
Huu ndio uswahili, kwawo najifakharisha

Sikusudii dhihaki, nachonga watu ukali
Nawataka washiriki, kwa hili kulijadili
Wanambe kwengine kupi, kwa uswahili asili
Huu ndio uswahili, kwawo najifakharisha.

Hamad Hamad
Aprili 26, 2011
Copenhagen

Leave a Reply

Fill in your details below or click an icon to log in:

WordPress.com Logo

You are commenting using your WordPress.com account. Log Out /  Change )

Facebook photo

You are commenting using your Facebook account. Log Out /  Change )

Connecting to %s

This site uses Akismet to reduce spam. Learn how your comment data is processed.